Mwili wa mwanamume huyo ulipatikana asubuhi ukinig’inia kwenye nguzo za transfoma hio huku nguo zake zikionekana kuwa zimeraruka.
OCPD wa Buruburu Richard Kerich alisema: “Mwanamume huyo alikanyaga nyaya zilizokuwa na umeme kupelekea kwake kuangukia nyaya zengine zenye umeme na kusababisha kifo chake.”
Mafuta ya transfoma yanaaminika kutumiwa katika kukaanga viazi ili kutengeza chipsi.
Polisi bado hawajabaini mtu huyo ni nani na mwili wake kupelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha jiji la Nairobi.
chanzo: jaridaleo
0 comments:
Post a Comment