Viongozi waanzisha harakati ya kupinga AlShabaab


Viongozi wa dini ya kiislamu kutoka jamii ya Kisomali humu nchini wameikashifu serikali kwa kufunga hawala zao licha ya wao kuhusika pakubwa katika kupiga vita mienendo ya kundi la Al-shabaab.

Viongozi wa dini ya kiislamu kutoka jamii ya Kisomali humu nchini wameikashifu serikali kwa kufunga hawala zao licha ya wao kuhusika pakubwa katika kupiga vita mienendo ya kundi la Al-shabaab.

Shekh Mohammed Osman amepuzilia mbali madai kuwa viongozi wa dini ya kiisilamu hawawajibiki kuzuia makundi yenye itikadi kali na kusisitiza kuwa serikali haioni juhudi zao.

Aidha wamepinga hatua ya  serikali ya kuhusisha misikiti na makundi yenye itikadi kali na kusema kuwa hatua hii inarudisha chini imani ya waislamu katika kupinga harakati za makundi ya kigaidi.

Wakizungumza baada ya kikao cha mashauriano jijini Nairobi, viongozi hao wameahidi kuanza kampeni ya kuhamasisha vijana dhidi ya makundi yenye itikadi kali kama njia ya kuepuka kujiunga na kundi la Al-shabaab.
Next PostNewer Post Previous PostOlder Post Home

0 comments:

Post a Comment