raudhwal islamic group
Mfanyibiashara maarufu Zadock Ainea Agutu na sheikh Ahmed Mursal ‘Sudan’ kutoka Mandera wamefikishwa mahakamani hii leo kwa madai ya kufadhili wanamgambo wa Al Shabaab.
Agutu alitiwa mbaroni katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta baada ya kuwasili kutoka Somalia.

Polisi wanadai kuwa wawili hawa wamekuwa na mawasiliano na washirika wakuu wa Al Shabaab akiwemo Mohammed Kuno maarufu Dulyadin ama Gamadhere anayesakwa na polisi kwa madai ya kuhusika na mauaji ya Garissa.
Serikali imeahidi kima cha shilingi milioni 20 kwa yeyote atakayetoa habari kuhusu Dulyadin.

Balozi wa Tanzania nchini Oman Mh. Ali Ahmed Saleh (aliyebeba mtoto) akiwa na baadhi ya kundi la Watanzania 18 waliookolewa kutoka Yemen ambako hakukaliki kutokana na vita. Hapa wananchi hao  wapo  katika uwanja wa ndege wa Muscat wakiwa njiani kurejeshwa nyumbani.


Viongozi wa dini ya kiislamu kutoka jamii ya Kisomali humu nchini wameikashifu serikali kwa kufunga hawala zao licha ya wao kuhusika pakubwa katika kupiga vita mienendo ya kundi la Al-shabaab.

Viongozi wa dini ya kiislamu kutoka jamii ya Kisomali humu nchini wameikashifu serikali kwa kufunga hawala zao licha ya wao kuhusika pakubwa katika kupiga vita mienendo ya kundi la Al-shabaab.

Shekh Mohammed Osman amepuzilia mbali madai kuwa viongozi wa dini ya kiisilamu hawawajibiki kuzuia makundi yenye itikadi kali na kusisitiza kuwa serikali haioni juhudi zao.

Aidha wamepinga hatua ya  serikali ya kuhusisha misikiti na makundi yenye itikadi kali na kusema kuwa hatua hii inarudisha chini imani ya waislamu katika kupinga harakati za makundi ya kigaidi.

Wakizungumza baada ya kikao cha mashauriano jijini Nairobi, viongozi hao wameahidi kuanza kampeni ya kuhamasisha vijana dhidi ya makundi yenye itikadi kali kama njia ya kuepuka kujiunga na kundi la Al-shabaab.


MAAFISA wa polisi mjini Nyahururu nchini Kenya usiku wa kuamkia Alhamisi walitibua mpango wa watu wasiojulikana wakionya jamii ya waislamu kuhama mjini humo.

Kulingana na mkuu wa polisi Nyandarua kaskazini Benjamin Onsongo, karatasi Zenye ujumbe wa kuwataka Waislamu waondoke mjini humo zilianza kusambazwa Jumapili iliyopita. 

Onsongo alisema ilani hiyo iliipa jamii hiyo makataa ya siku saba kuhama mji huo kwani wamekataa kutambulisha maadui wanaoivamia nchi ya Kenya.

“Tumeanzisha uchunguzi na tumewaongeza maafisa wa polisi wanaoshika doria katika eneo hilo na nina uhakika kuwa tutawatia mbaroni wahusika,” alisema Bw Onsongo.

Viongozi wa kiislamu wakiongozwa na Imam wa msikiti wa Jamia mjini Nyahururu Sheikh Mohamed Huka pamoja na mwenyekiti wa muungano wa Waislamu kaunti ya Laikipia Sheikh Isaack Osman waliambia jamii ya waislamu mjini humu kutoogopeshwa na ilani hizo kwani maafisa wa polisi wanalishughlikia suala hilo.

Sheikh Mohamed Huka wa msikiti wa Jamia, Nyahururu akiwa na moja
ya vijikaratasi vilivyosambazwa mji wa Nyahururu Alhamisi vikiwataka watu wa
dini ya Kiislamu wahame mji huo
“Karatasi hizi zinasambazwa na watu wachache ambao wanataka kututawanya kwa misingi ya kidini lakini hatutakubali kugawanywa, ninaamini kuwa Nyahururu ni mji wa amani,” alisema Osman.

Sheikh Huka alisema kuwa jamii ya Waislamu imekubali kukumbatia mfumo wa Nyumba Kumi ili kuinua usalama na kuwauliza kuwa na subira huku maafisa wa polisi wakiendeleza uchunguzi


Hatimaye kundi la kwanza lililo na wakenya 15 waliyokuwa nchini Yemen wanatarajiwa kuwasili katika uwanja wa jomo kenyetta hii leo.

Kulingana na mkuregenzi wa masuala ya mataifa ya kigeni humu nchini Washington Oloo ni kuwa serikali imekuwa ikiwasiliana na mataifa ya china na India ilikusaidia kuwahamisha wakenya kutoka maeneo yaliyo athirika zaidi na ghasia.

Oloo ameongeza kwa kusema kuwa zaidi ya wakenya 5000 wamekwama katika taifa la yemen huku 53 wakitorokea nchi jirani ya Saudi Arabia.

Aidha takriban wakenya 250 wanaishi katika vitongoji vya mji mkuu wa Sanaa nchini humu ikilinganishwa kuwa ni moja la eneo lilikumbwa na vita hivyo.

Itakumbukwa kuwa mwanzoni mwa mwezi huu maeneo mengi nchini Yemen yameweza kuathirika na ghasia.


somalissssss
Hatimaye shughli za ujenzi wa ukuta wa mpaka wa Kenya na Somali umeanzishwa rasmi hii leo katika eneo la Kiunga kaunti ya Lamu.

Ujenzi huo umeanzishwa rasmi na kushuhudiwa na kamishna mkuu wa lamu Fredrick Ndambuki.

Aidha Ndambuki amesema kuwa madhumuni ya ujenzi huo ni kulinda usalama na kuthibiti mashambulizi yanayo tekelezwa na kundi la wapiganaji la Al-shabaab.

Hatahivyo ameonyesha matumaini ya kuwepo amani na usalama katika taifa la Kenya.
Previous PostOlder Posts Home