Waziri wa Mifugo na Uvuvi Zanzibar Mhe Abdilah
Jihad Hassan amesema kuwa Serikali itaendelea kuandaa mazingira bora ya
wavuvi ikiwa ni pamoja na kujenga masoko ya kisasa ili kuimarisha
sekta ya uvuvi na kuzalisha ajira kwa wananchi .
Amesema kuwa wananchi wengi wa Visiwa vya Zanzibar
wanategemea sekta ya Uvuvi kuendesha shughuli zao za uchumi na kueleza
kwamba jumla ya watu 34,000 wamejiajiri kupitia sekta ya uvuvi ambapo
kupatikana kwa masoko ya kisasa kutaongeza ajira kwa wananchi .
Kauli hiyo ameitoa wakati akikabadhi soko la Tumbe Wilaya ya Micheweni kwa Mkuu wa Mkoa wa Kaskazni Pemba , ambalo limejengwa na kampuni ya Ngogo ya Iringa na kugharimu zaidi ya shilingi milioni 712.
Aidha waziri jihad amewataka wananchi wa Wilaya ya Micheweni kulitumia soko hilo kwa kufuata mila , silka na tamaduni wa watu wa Tumbe .
Kauli hiyo ameitoa wakati akikabadhi soko la Tumbe Wilaya ya Micheweni kwa Mkuu wa Mkoa wa Kaskazni Pemba , ambalo limejengwa na kampuni ya Ngogo ya Iringa na kugharimu zaidi ya shilingi milioni 712.
Aidha waziri jihad amewataka wananchi wa Wilaya ya Micheweni kulitumia soko hilo kwa kufuata mila , silka na tamaduni wa watu wa Tumbe .
“Tunatambua kwamba soko hili
liko sehemu za mkusanyika wa watu wengi kutoka sehemu tofauti za Pemba ,
hivyo basi mnatakiwa kusimamia na kufuata mila , silka na tamaduni za
wenyeji wa hapa ili kusiwepo na mporomoko wa maadili ya jamii ”
alisisitiza Jihad .
Mapema Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mhe Omar Khamis Othman
amewashauri wavuvi wa Wilaya ya Micheweni kuhamasishana kulitumia soko
hilo ili liweze kutumika na kukuza uchumi wao na Taifa kwa Ujumla .
Mkuu huyo wa Mkoa
ameitaka Wizara ya Mifugo na Uvuvi kutoa kipaombale cha kwanza kwa
wakaazi wa Tumbe nakushauri kwamba uteuzi wa vijana kujiunga na chuo cha
Uvuvi zielekezwe kwa wakaazi wa Tumbe .
” Hizi nafasi za
vijana kujiunga na chuo cha Uvuvi ambazo Wizara mmeanza kuzitoa
naomba vijana wa Tumbe nao wapewe kipaombele cha pekee ili kuwafanya
wakiridu waweze kuliboresha soko hili ” alishauri Mkuu wa Mkoa .
Akitoa taarifa za ujenzi wa Soko hilo Katibu Mkuu wa Wizara ya
Mifugo na Uvuvi Bw Kassim Gharib Juma amesema kuwa katika kipindi cha
mwaka 2014 jumla ya Tani 30,000 wenye thamani ya bilioni 106 na
wamevuliwa Unguja na Pemba .
Amesema kuwa lengo la
Serikali ni kuwafanya vijana kujiajiri wenyewe kupitia sekta ya Uvuvi na
tuko mbioni kukamilisha mipango ya kuwaandaa wavuvi kuweza kufikia
bahari kuu kwa ajili ya uvuvi .
Ameeleza kwamba hilo
litafikiwa kutokana na azma za Rais Shein za kutoka kuiboresha sekta ya
Uvuvi kwa kuwapatia vifaa na dhana za kisasa za uvuvi ambazo zitawafanya
walitumie eneo la bahari kuu .
0 comments:
Post a Comment