Waziri Duni afungua kituo kipya cha kununulia karafuu, Kilindi , Chake


 
WAZIRI wa Miundombinu na Mawasiliano Zanzibar, Mhe: Juma Duni Haji akiondoa kitambaa kuashiria kufungua kituo kipya cha kununulia karafuu, kilichopo Kilindi wilaya ya Chake Chake Pemba, kilichojengwa na ZSTC, ikiwa ni shamra shamra ya kutimia miaka 51 ya mapinduzi Zanzibar, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

 BAADHI ya wananchi wa shehia ya Kilindi wilaya ya Chake Chake Pemba, wakimsilikiza Mkurugenzi mtendaji wa ZSTC Zanzibar, Mwahija Al-masi Ali akizungumza kwenye ufunguzi wa kituo kipya cha kununulia karafuu kwenye shehia hiyo, ikiwa ni shamra shamra ya kutimia miaka 51 ya mapinduzi Zanzibar, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 
KIKUNDI cha burudani cha Mkota ngoma cha Mkoani Pemba, kikitumbuiza kwa ngoma ya kibati, kwenye ufunguzi wa kituo kipya cha ununuzi wa karafuu shehia ya Kilindi wilaya ya Chake Chake Pemba, ikiwa ni shamra shamra ya kutimia miaka 51 ya mapinduzi ya Zanzibar, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

WAZIRI wa Miundombinu na Mawasiliano Zanzibar, Mhe: Juma Duni Haji, akizungumza  na wananchi wa shehia ya Kilindi wilaya ya Chake Chake Pemba, mara baada ya kukifungua kituo kipya cha kununulia karafuu, kilichopo shehiani humo, ambacho kilijengwa na ZSTC, ikiwa ni shamra shamra ya kutimia miaka 51 ya mapinduzi Zanzibar, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 

Next PostNewer Post Previous PostOlder Post Home

0 comments:

Post a Comment